Wednesday, April 16, 2008

Mjadala wa Maendeleo Ubungo-12 April 2008

Mjadala wa Maendeleo Ubungo ulikwenda vizuri tarehe 12 Aprili 2008. Watoa mada siku hiyo walikuwa ni Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni(huduma zitolewazo na manispaa); Mstadi toka kampuni ya TESTA(Huduma zitolewazo na asasi za kiraia) na Mmoja wa waasisi wa UDI. Mkurugenzi wa UDI naye alihutubia siku hiyo. Tutawaletea mada za wazungumzaji wote pamoja na ripoti ya mjadala huo ikiwa tayari. Kwa leo, tuwawekee mada moja wapo:

Mada iliyowasilishwa kwenye Mjadala wa Maendeleo-Jimbo la Ubungo uliofanyika katika Ukumbi Wa Land Mark Hotel, Ubungo-Dar es salaam. Mwandishi wa mada hii ni mwanaharakati, mkazi wa jimbo la Ubungo na mmoja ya waasisi wa Asasi ya Maendeleo Ubungo (UDI) anayepatikana kupitia 0754694553 na mnyika@yahoo.com


USHIRIKI WA WANANCHI KATIKA KULETA MAENDELEO

“MISINGI 25”

Na John J. Mnyika

Mada hii imeandaliwa kwa ufupi kuchochea fikra na mjadala kuhusu “Ushiriki wa Wananchi Katika Kuleta Maendeleo”; na haki/wajibu katika muktadha huo hususani kwa viongozi na wananchi wa Jimbo la Ubungo.

Yapo masuala na mahitaji mengi ambayo kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuyafanya katika kuleta maendeleo katika eneo lake.
• Eneo inaweza kuwa ni asasi/taasisi, kijiji/mtaa, jimbo/wilaya nk.
• Ieleweke kwamba maendeleo yanayozungumzwa hapa si maendeleo ya mtu binafsi bali ni maendeleo ya jumuia/jamii.
• Kiongozi na mwananchi wa jimbo la Ubungo anayelengwa hapa inaweza kuwa kiongozi wa asasi/kikundi, mwanaharakati wa kawaida, kiongozi aliyechaguliwa na wananchi(mfano mwenyekiti wa kijiji, diwani) nk.


Masuala na mahitaji hayo yako katika sehemu kadhaa mathalani haki, wajibu, zana, mikakati, maangalizo, dondoo, stadi, mazingatio, shughuli na kadhalika. Mada hii imeyaweka pamoja masuala na mahitaji hayo kwa pamoja katika mtiririko rahisi na kuyaita jina la pamoja “Misingi 25”. Hivyo misingi iliyoainishwa hapa ni sehemu ya mambo muhimu ambayo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuyafanya yaweze kumsadia katika kuleta maendeleo katika eneo lake.

Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuzingatia misingi ifuatayo ili kuleta maendeleo:

I. UPATAJI WA RASLIMALI: Upataji wa raslimali na suala la msingi ambalo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kulifahamu na kulitilia maanani. Hii ni kwasababu maendeleo huletwa na kuwekeza raslimali. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa afahamu aina, vyanzo na namna ya kupata raslimali. Raslimali ni pamoja na watu, fedha, vitu na hata mawazo. Vyanzo vya raslimali vyaweza kuwa wananchi, serikali, wadau wa kimaendeleo, mashirika yasiyo ya kiserikali nk. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ni vyema akawa na stadi au akatumia wenye stadi za uandishi wa miradi na ukusanyaji wa raslimali. Baadhi ya vyanzo muhimu vya kiserikali ni pamoja na: Pesa za Maendeleo (capital development fund) ambazo zinatolewa kwa idadi ya watu kwa wastani wa dola moja na nusu kwa kila kichwa katika kata; Pesa za PADEP-Participatory Agricultural Development Programme(hizi zinatolewa kwa ajili ya miradi ya kijamii na miradi ya vikundi); Pesa za VVU/UKIMWI kupitia TACAIDS; pesa za mradi wa elimu ya msingi-MMEM; pesa za mpango wa elimu ya sekondari-MMES, pesa za TASAF-miradi ya vijiji/mitaa na mikopo kwa vikundi na vyanzo vingine vingi. Hivi vinashindwa kutumika baadhi ya maeneo kutokana na kutokufahamika ama kutokufuatiliwa ipasavyo. Baadhi ya vyanzo vya washirika wengine wa kimaendeleo ni PACT, SATF, Foundation for Civil Society, GTZ, USAID, FHI, DFID, CARE nk. Kuna haja ya kufuatilia kujua taratibu za kupata ruzuku au kujenga ushirika na taasisi hizi.


II. USHAWISHI NA UTETEZI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na stadi za ushawishi na utetezi. Hizi ni zana muhimu sana kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kutekeleza wajibu wa kuleta maendeleo. Uzoefu unaonyesha kuwa kuna viongozi ama wananchi wa Ubungo ambao wameweza kuleta maendeleo katika maeneo yao kutokana na kutumia vizuri stadi hizi. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo unapaswa kuelewa kuwa ‘ukitaka kuwamba ngoma lazima uvutie upande wako’. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutumia kila fursa ya vikao na nafasi nyinginezo kushawishi miradi ya kimaendeleo kuelekezwa katika kufanyika katika eneo lake. Utetezi unahusisha pia kuweza kujenga hoja katika medani mbalimbali kwa niaba ya wananchi wenye matatizo mbalimbali. Stadi za ushawishi na utetezi zinawezesha kujua wajibu huu unatekelezwa namna gani.

III. UHAMASISHAJI NA KAMPENI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na ufahamu wa jinsi ya kufanya uhamasishaji na kampeni. Huu ni msingi muhimu katika kuunganisha nguvu za viongozi na wananchi kwa ujumla. Pia hii ni zana muhimu katika kutatua masuala yanayokabili halaiki ya wananchi yanayohusika na kubadili fikra na mitazamo. Mathalani Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo lazima awe mstari wa mbele katika kupiga vita UKIMWI. Pia awe mstari wa mbele kuhamasisha wananchi kutumia fursa mbalimbali zinazojitokeza. Kufanya mikutano ya jumuia ni wajibu wa msingi wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kama sehemu ya kufanikisha malengo haya.

IV. UFAHAMU WA SHERIA ZA MSINGI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na ufahamu wa sheria za msingi. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo wananchi mara kadhaa wanamtegemea Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwapa mwelekeo katika maeneo hayo. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu sheria za msingi. Si lazima Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwa na ufahamu wa kina wa kisheria maana anaweza kutumia misaada mbalimbali ya kisheria katika masuala tata lakini unapaswa kufahamu masuala la msingi kwa ajili ya kutoa mwelekeo.

V. UFAHAMU WA SERA ZA MSINGI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu masuala ya msingi ya kisera. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu sera za kiserikali yanayogusa moja kwa moja makundi maalumu ama wananchi kwa ujumla katika eneo husika kwa kuwa ni msingi wa muhimu katika kuundaa miradi ya kimaendeleo na kujenga hoja za kupata raslimali katika maeneo hayo.

VI. UPANGAJI WA MIPANGO: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na stadi za msingi za kupanga mipango au kuwatumia vizuri wataalam. Baadhi ya stadi za msingi ni pamoja na maandalizi ya mapendekezo ya miradi, kuandaa mipango kazi na kutayarisha mipango kazi. Katika mazingira ya sasa, raslimali ziko nyingi na zinapatikana kwa ushindani. Uwezo wa kupanga mipango inayotimiza vigezo ni msingi muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweza kutelekeleza wajibu wa kuleta maendeleo. Pia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuielewa mipango iliyopo ikiwemo ya serikali ambayo inaigusa eneo lake kwa namna moja au nyingine.

VII. UPANGAJI WA BAJETI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuelewa michakato ya upangaji wa bajeti hususani bajeti. Hii ni kwa sababu bajeti ni zana inayoongoza mgawanyo na matumizi ya raslimali. Hivyo maendeleo ya eneo lake inategemea vilevile kiasi ambacho eneo husika linapangiwa katika bajeti za ujumla. Uwezo wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kushawishi bajeti kuelekezwa katika eneo lake inategemea ujuzi na ushiriki katika katua za muhimu za kupanga bajeti.

VIII. UUNDAJI WA ASASI NA VIKUNDI VYA MAENDELEO: Katika muelekeo wa sasa wa kimaendeleo vikundi vinachukuliwa na serikali na wadau mbalimbali kama njia ya msingi ya kuleta maendeleo hususani katika ngazi za chini. Hivyo katika kuzitumia fursa hizi ni muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwa na uwezo wa kuhamasisha vikundi vidogo vidogo kuundwa katika eneo lake hususani na wanawake na vijana. Vikundi vinaweza kuundwa kulingana na mahitaji lakini ni muhimu kukawa na vikundi vya kuweka na kukopa pamoja na vikundi vya uzalishaji mali. Ni muhimu pia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwa na asasi ya kijamii(CBO) ya katika eneo lake ambayo atashiriki na kuitumia kama mwanya wa kuvuta raslimali ambazo ni mahususi kwa ajili ya mashirika yasiyo ya kiserikali.

IX. KUTUMIA UZOEFU WA MAENEO MENGINE: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ni muhimu kuamua kwa dhati kutumia uzoefu wa maeneo mengine. Kuna msemo kwamba hakuna haja ya kugundua gurudumu kama gurudumu lipo tayari. Msemo huu unamtaka Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuchota uzoefu katika maeneo mengine. Yapo maeneo ambayo viongozi ama wananchi wa Ubungo wake wametekeleza wajibu wa kuleta maendeleo kwa namna ya kuigwa. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kubadilishana uzoefu na viongozi wa maeneo hayo ama kwa kutembelea au kwa mawasiliano au kwa kusoma ripoti mbalimbali za msingi.


X. KUTUMIA WANACHAMA: Pamoja na kutumia chama/kikundi/asasi kama taasisi. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo lazima aweke kipaumbele kuwatumia wanachama wa chama/kikundi/asasi. Hii ni kwasababu wanachama wana shauku ya ziada kushiriki katika kuhakikisha Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anafanikiwa ili chama/kikundi/asasi kiweze kujijengea heshima na kukubalika. Hivyo kushiriki katika shughuli za chama/kikundi/asasi ni hatua ya msingi kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweza kuwa karibu na wanachama na hatimaye wanachama kwa upande wao kuweza kujitolea katika kuwaunga mkono.

XI. KUTUMIA WATAALAMU: Si misingi yote iliyotajwa humu ambayo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo atakuwa na utaalamu. Hivyo ni muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuamua kwa dhati kuwatumia wataalam mathalani katika kuandaa mipango, kuandika miradi nk. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo asione aibu kuhusisha wataalamu.Kushirikisha wataalamu kamwe si ishara ya udhaifu wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo. Ni suala la mgawanyo wa majukumu kati ya yale ya kitaalamu na majukumu ya kawaida ya kiuongozi.


XII. KUTUMIA MAWASILIANO: Uwezo wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kutumia mawasiliano ni msingi muhimu katika kufanikishwa wajibu wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo katika kuleta maendeleo. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu njia mbalimbali za mawasiliano na jinsi ya kuzitumia kwa ufanisi. Njia rahisi tu kama kuandika barua kwa mamlaka zinazohusika na wadau mbalimbali katika kuhamasisha maendeleo katika eneo lake inaweza kufanya maajabu. Hata hivyo kwa masuala makubwa na vyema Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo akatumia njia za mawasialiano ya umma kwa mfano kubandika matangazo na kufanya mikutano ya jumuia. Lakini pale yanapotokea matatizo makubwa ni vyema kutumia hata vyombo vya habari pale vinapoweza kufika. Mathalani tatizo la njaa katika kata likitoka katika vyombo vya habari mamlaka zinazohusika zinaweza kuingilia kati kwa haraka zaidi kuliko mawasiliano ya chini kwa chini.


XIII. STADI ZA MAHUSIANO: Stadi za mahusiano (interpersonal skills) ni msingi muhimu sana kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweza kuleta maendeleo. Hii ni kwa sababu ukaribu wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo na watu mbalimbali ni hatua muhimu sana katika kuvutia mipango ya kimaendeleo. Pia baadhi ya miradi hutegemea mahusiano ya ukaribu kati ya Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo na wadau wa maendeleo pamoja na watendaji katika asasi hizo. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo achukulie ukaribu kama daraja la kupata fursa za kimaendeleo katika eneo lake.

XIV. KUJENGA MTANDAO NA USHIRIKA: Kuna umuhimu wa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kujenga mtandao na ushirika (network and coalition) hususani na viongozi ama wananchi wa Ubungo wengine ambao wanakubaliana katika ajenda/mipango/malengo. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo achambue masuala yanayogusa kata za jirani na kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha yanafanikiwa. Hii ni muhimu katika kujenga nguvu ya pamoja katika kushughulikia masuala mbalimbali ya kimaendeleo. Pia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ajenge mtandao na ushirika na watu muhimu katika eneo lake, hii inasaidia sana katika kuongeza nguvu katika kushughulikia masuala la kimaendeleo.

XV. KUTUMIA WADAU WENGINE: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuelewa nguvu iliyoko katika kuwatumia wadau wengine. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuanza kwa kutambua wadau muhimu waliopo katika eneo lake na maeneo jirani. Lakini pia anapaswa kuwaelewa wadau wa nje ambao wanaweza kushawishiwa kufanya kazi katika eneo lake. Hii ni muhimu kwa sababu uzoefu unaonyesha kuwa kuna miradi mingi ya kimaendeleo ambayo inametekelezwa katika maeneo mbalimbali na wadau kama asasi zisizo za kiserikali, mashirika ya dini na kadhalika.

XVI. KUELEWA MIPANGO YA KISERIKALI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuielewa mipango mbalimbali ya kiserikali. Hii ni hatua muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweza kuhakikisha mipango hii inatekelezwa katika eneo lake. Baadhi ya mipango ya kiserikali ambayo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu michakato yake ni pamoja na: Mpango wa uwezeshaji kuanzia vijijini(mipango shirikishi inapangwa vijijini, WDC zinapeleka katika halmashauri-ni muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuhakikisha mipango shirikishi inapangwa ambayo ndio msingi wa bajeti);


XVII. UMUHIMU WA VIKAO: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu nguvu ya vikao katika kuleta maendeleo. Hii ni kwa sababu masuala mengi ya kimaendeleo yanahitaji maamuzi ambayo hufanyika katika vikao. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na utaratibu wa kuitisha vikao au mikutano na wanachama/wananchi kwa ajili ya kuchukua maoni, kutoa taarifa ama kujenga ukaribu. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa pia kuhakikisha kuwa anahudhuria vikao vyote muhimu anavyopaswa kuhudhuria ili kuhakikisha maslahi ya eneo lake yanazingatiwa. Kwa upande mwingine Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ahakikishe vikao vya kimaendeleo katika eneo lake vinakaa. Hivi ni vikao ambavyo vinafanya maamuzi ya msingi sana kwa ajili ya maendeleo. Ni muhimu akahudhuria vikao vya madiwani(full council) ambavyo wananchi wa kawaida wanaruhusiwa kuhudhuria.

XVIII. KUEPUKA VIKWAZO VYA KITAASISI: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na uwezo wa kuvuka vikwazo vya kitaasisi ikiwemo vya kiserikali katika kuleta maendeleo. Vikwazo viko vya namna mbalimbali mathalani urasimu, kutopewa kipaumbele, tofauti zinazotokana na misimamo nakadhalika. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuwa na mbinu za kukabiliana na vikwazo hivi. Mbinu ya msingi ni kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kufahamu vizuri haki na wajibu wake pamoja na kujua jinsi sheria na sera zinazomlinda. Pia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ajenge ukaribu na baadhi ya watendaji/wataalamu katika taasisi/serikali ili waweze kumuunga mkono. Kwa upande mwingine wale watendaji wanaoweka vikwazo lazima kuchunguza udhaifu wao na kuwabana katika udhaifu wao na kuwafanya watimize wajibu kwa hofu. Wakivuka mipaka Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anao uwezo wa kupeleka hoja wakaondolewa. Kuunganisha nguvu na wadau wengine ni njia ya ziada ya Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuruka vikwazo. Pia unaweza kutumia viongozi wa juu zaidi. Vikwazo vikifikia hatua ya juu zaidi ni vyema kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweka mambo bayana kupitia vyombo vya habari ama njia nyinginezo ili taasisi au serikali kwa ujumla wake iweze kutambua na kurekebisha hali hiyo. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutambua kuwa cha muhimu ni ujasiri. Kwenye kufuatilia haki hakuna kurudi nyuma na wakati mwingine haki haiombwi-inadaiwa.


XIX. USHIRIKI, USHIRIKISHAJI NA USHIRIKISHWAJI: Hizi ni dhana zinazorandana ambazo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuzitumia. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anao wajibu wa kushiriki katika michakato ya maendeleo. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuelewa kuwa ushiriki wake ni hatua muhimu kwa michakato hiyo kufanikiwa. Lakini pia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutulia mkazo kuwashirikisha wanachama/wananchi na wadau wengine kama msingi muhimu wa kuunganisha nguvu za pamoja. Kwa upande mwingine Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ahakikishe kwamba anashirikishwa katika mahali ambapo ni muhimu kwake lakini kwa namna moja au nyingine amesahaulika.

XX. KUJENGA IMANI KUPITIA UKWELI, UWAZI NA UWAJIBIKAJI: Kwa ujumla wanachama/wananchi na wadau wengine wa kimaendeleo katika maeneo mbalimbali wamepoteza imani na baadhi ya viongozi. Hii inawafanya wasiunge mkono kikamilifu masuala ya kimaendeleo yanayoratibiwa na viongozi hao ikiwemo katika baadhi ya maeneo kutotoa michango ya kutosha katika shughuli za kimaendeleo. Hii ni changamoto kwa viongozi na wananchi wa Ubungo. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutambua kuwa njia ya msingi ya kukabiliana na hali hii ni kujenga imani kupitia ukweli, uwazi na uwajibikaji. Kuhakikisha pesa zinatumika kwa uaminifu ni nguzo muhimu sana ya kumwezesha Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuhakikisha raslimali nyingi zaidi za kimaendeleo zinapatikana katika eneo lake.


XXI. NGUVU YA UBUNIFU NA KUCHUKUA HATUA: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu kuwa katika mazingira ya sasa ya ushindani ubunifu ni msingi wa muhimu wa kufanikiwa katika kuleta maendeleo. Mathalani pesa nyingi za miradi ya maendeleo zinatolewa kwa ushindani. Pia wakati mwingine wananchi wa eneo lake wanamtegemea Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kama kiongozi anayepaswa kutoa fikra mpya kuhusu muelekekeo wa kimaendeleo katika eneo lake. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutekeleza msingi huu. Si lazima ubunifu wote utokane na yeye, Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anaweza kuchota mawazo toka kwa watu wengine na kuyatoa katika sura yenye kuchochea mwamko na kuungwa mkono. Lakini mawazo ya ubunifu pekee hayawezi kuleta maendeleo kama hayatekelezwi. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuhamasisha na kuchochea mawazo ya ubunifu yawezwe kuwekwa katika mipango na hatimaye kutelezwa. Hivyo kuchukua hatua na kufuatilia ni nyenzo za muhimu kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuweza kuzitumia. Ukitaka kuanzisha miradi lenga katika ile inayoonekana. Na wakati wote jitahidi kuanza kwa raslimali watu. Miradi mingi inatumia mfumo wa “changa, uchangiwe”, hivyo ni vyema Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwa mbunifu wa kuanza.

XXII. KIONGOZI AMA MWANANCHI WA UBUNGO KUWA MSTARI WA MBELE NI FAIDA: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutambua kwamba uongozi na mwananchi kuwa mstari wa mbele ni faida na kwa hivyo kutekeleza wajibu kwa moyo wote na hatimaye kuleta maendeleo. Kwa upande mmoja uongozi na uanaharakati ni faida kwa jamii kwani kwa kupitia Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo maendeleo/mabadiliko yanaweza kupatikana ambayo ni manufaa kwa jamii ya sasa na jamii ya baadaye. Kwa upande mwingine uongozi na harakati ni faida kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo mwenyewe, hii ni kwa sababu inamwezesha kutambulika katika jamii, kukutana na watu/asasi mbalimbali, kupata ufahamu na kupata fursa mbalimbali za ziada.


XXIII. TUMIA MIFUMO/MIUNDO ILIYOPO: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuweka mkazo katika kuitumia mifumo/miundo iliyopo. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo aanze kwa kuchambua ni mifumo/miundo gain iliyoko katika eneo lake ambayo anaweza kuitumia. Ukweli ni kuwa katika eneo lake na nchi yetu kwa ujumla iko miundo/mifumo mingi ambayo haitumiki. Kutumia mifumo/miundo iliyopo kutamwezesha Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kupata matokeo ya kimaendeleo kwa haraka na nafuu zaidi bila kupoteza muda na raslimali za kuanzisha ama kushawishi mifumo mingine.


XXIV. NGUVU YA HOJA: Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kutambua kwamba nguvu ya hoja ni mhimili muhimu katika kufanikisha misingi yote muhimu ya kuleta maendeleo. Nguvu ya hoja inawezesha mawazo ya kimaendeleo kueleweka na kutekelezwa. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ajenge utamaduni wa kuhakikisha hoja zake zinakuwa na uzito. Ili kuwa na nguvu ya hoja ni lazima kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kuwa na taarifa za msingi mara kwa mara. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo awe mchunguzi ama mfuatiliaji. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo asiogope uchache mathalani wakati ambapo suala analolisimamia halijatokana na hoja iliyoletwa na wengi. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kufahamu kuwa cha muhimu ni nguvu ya hoja ambayo inaweza kutengeneza nguvu ya kuungwa mkono. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anapaswa kuhakikisha anazungumza kitu chenye uhakika ili kuepuka kudharauliwa au pengine hata kuchukuliwa hatua. Suala la msingi kwa Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo kusoma-sheria, kanuni, taratibu na nyaraka mbalimbali.

XXV. ENEZA TAARIFA NA ELIMU YA URAIA: Ukichambua kwa makini utagundua kuwa chanzo kikuu cha matatizo mengi miongoni mwa wananchi ni kukosa taarifa ama elimu ya uraia. Wapo wananchi wanaonyanyashwa kwa kushindwa tu kujua haki zao, wapo wanaokosa fursa za kielimu kwa kushindwa kujua wapitie hatua zipi, wapo wajane wanaonyang’anywa mirathi kwa kushindwa tu kujua jinsi ya kusimamia stahili zao, wapo waopoteza maisha kwa magonjwa kutokana na kukosa tu taarifa za msingi nakadhalika. Hivyo yapo maendeleo ambayo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo anaweza kuyaleta kwa kuwezesha tu taarifa za msingi na elimu ya uraia kuenea kwa wananchi wengine. Hivyo Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo aweke mkazo kwa namna ya pekee sana kuhakikisha taarifa zinaenea na elimu ya uraia inatolewa. Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo awe mstari wa mbele katika kufanikisha msingi huu kupitia mikutano ya jumuia, vipeperushi na njia nyinginezo. Kwa upande mwingine Kiongozi ama mwananchi wa jimbo la Ubungo ahakikishe wadau wengine ikiwemo serikali wanatoa taarifa muhimu na kueneza elimu ya uraia kuhusu fursa na michakato mbalimbali ya kimaendeleo.

Rejea:

• John Mnyika, Misingi 29 ya Vijana Kuleta Maendeleo Katika Maeneo yao-2007
• Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977
• Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu, 1948(UDHR).
• Ushiriki wa Wananchi katika Serikali za Mitaa, 2005(Policy Forum)
• Sheria ya Serikali za Mitaa, 1982

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home